Psalms 96:1-6

Mungu Mfalme Mkuu

(1 Nyakati 16:23-33)


1 aMwimbieni Bwana wimbo mpya;
mwimbieni Bwana dunia yote.

2 bMwimbieni Bwana, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

3 cTangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.


4 dKwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

5 eKwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Bwana aliziumba mbingu.

6 fFahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

Copyright information for SwhKC