Psalms 96:1-6
Mungu Mfalme Mkuu
(1 Nyakati 16:23-33)
1 aMwimbieni Bwana wimbo mpya;
mwimbieni Bwana dunia yote.
2 bMwimbieni Bwana, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 cTangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 dKwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 eKwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 fFahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Copyright information for
SwhKC